Forum Replies Created

Viewing 1 post (of 1 total)
  • Author
    Posts
  • Matho Lilian
    Moderator

    KANUNI/SHERIA ZA JUKWAA LA ANDIKA NA SOMA

    1. Kila mmoja ana haki ya kujiunga na jukwaa hili.

    2. Kila mwanajukwaa ana haki na uhuru wa kuchangia mada ikiwa ni pamoja na kutoa mawazo yake, hivyo ni lazima Mawazo yake yaheshimike/yaheshimiwe na kuthaminiwa. Majadiliano ndani ya jukwaa yataendeshwa kwa Uhuru bila kuzuia haki ya mchangiaji kutoa mawazo yake.

    3. Haitaruhusiwa kutoa taarifa za uongo zisizo thibitika.

    4. Jukwaa halitaegemea kwenye itikadi yeyote ya kisiasa wala dini.
    5. Mchangiaji hatoruhusiwa kutumia lugha yenye matusi, kukera, kuudhi ama kuchefua na kukejeli wengine. Lakini utani kama sehemu ya utamaduni wetu hautachukuliwa kama ni kejeli.

    7. Michango ya Mijadala ilenge Mada husika inayojieleza katika kichwa cha habari cha Mada husika, mpya ianzishwe kichwa cha habari kipya.

    8. Sheria na taratibu zingine ni Universal zinazoongoza majukwaa yote ya mitandao , kama utumiaji wa HERUFI KUBWA katika kujadili mada usiwepo.

    Moderator

Viewing 1 post (of 1 total)