Tone la Damu na Hadithi Nyingine

Tone la Damu na Hadithi Nyingine ni mkusanyiko wa hadithi kumi (10) bora za mzunguko wa tano (5) 2018 wa Andika na Soma, shindano la hadithi fupi kwa wanafunzi wa shule za sekondari Tanzania. Shindano hili lilibuniwa na kuendeshwa na Taasisi ya Usomaji na Maendeleo –Soma ili kuibua na kuchipuza vipaji vya uandishi wa kubuni miongoni mwa vijana; kuamsha ari ya usomaji na uandishi; na kuwawezesha vijana kutumia uandishi wa kubuni kujadili masuala yanayowahusu wao, jamii zao, taifa na ulimwengu.